38 Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.
39 Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.
40 Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.
41 Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.
42 Niliwatwanga wakawa kama vumbi inayopeperushwa na upepo;niliwakanyaga kama tope la njiani.
43 Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,ukanifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.
44 Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.