44 Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.
45 Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.
46 Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wa usalama wangu;atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.
47 Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.
48 Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,akanikuza juu ya wapinzani wangu,na kunisalimisha mbali na watu wakatili.
49 Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.
50 Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.