3 Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;tutupilie mbali minyororo yao!”
4 Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni,anawacheka na kuwadhihaki.
5 Kisha, anawakaripia kwa ghadhabu,na kuwatisha kwa hasira, akisema:
6 “Nimemtawaza mfalme niliyemteua,anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!”
7 Mfalme asema: “Nitatangaza azimio la Mwenyezi-Mungu.Mungu aliniambia:‘Wewe ni mwanangu,mimi leo nimekuwa baba yako.
8 Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,na dunia nzima kuwa mali yako.
9 Utawaponda kwa fimbo ya chuma;utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”