25 Kwa sababu yako ninakusifukatika kusanyiko kubwa la watu;nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.
26 Maskini watakula na kushiba;wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu watamsifu.Mungu awajalie kuishi milele!
27 Ulimwengu wote utakumbuka na kumrudia Mwenyezi-Mungu;jamaa zote za mataifa zitamwabudu.
28 Maana Mwenyezi-Mungu ni mfalme;yeye anayatawala mataifa.
29 Wenye kiburi wote duniani watasujudu mbele yake;wote ambao hufa watainama mbele yake,wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30 Vizazi vijavyo vitamtumikia;watu watavisimulia habari za Mwenyezi-Mungu,
31 watatangaza matendo yake ya wokovu.Watu wasiozaliwa bado wataambiwa:“Mwenyezi-Mungu ndiye aliyefanya hayo!”