6 Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,maana amesikiliza ombi langu.
7 Mwenyezi-Mungu ndiye nguvu yangu na ngao yangu;tegemeo la moyo wangu limo kwake.Amenisaidia nami nikashangilia kwa moyo;kwa wimbo wangu ninamshukuru.
8 Mwenyezi-Mungu ni nguvu ya watu wake;yeye ni kimbilio la wokovu kwa mfalme wake mteule.
9 Ee Mungu, uwaokoe watu wako;uwabariki watu hao walio mali yako.Uwe mchungaji wao na kuwategemeza milele.