5 Hasira yake hudumu kitambo kidogo,wema wake hudumu milele.Kilio chaweza kuwapo hata usiku,lakini asubuhi huja furaha.
6 Mimi nilipofanikiwa, nilisema:“Kamwe sitashindwa!”
7 Kwa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu,umeniimarisha kama mlima mkubwa.Lakini ukajificha mbali nami,nami nikafadhaika.
8 Nilikulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;naam niliomba dua kwako ee Mwenyezi-Mungu:
9 “Je, utapata faida gani nikifana kushuka hadi kwa wafu?Je, mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?Je, yanaweza kusimulia uaminifu wako?
10 Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, unihurumie;ee Mwenyezi-Mungu, unisaidie!”
11 Wewe umegeuza maombolezo langu kuwa ngoma ya furaha;umeniondolea huzuni yangu, ukanizungushia furaha.