1 Heri yake mtu aliyesamehewa kosa lake,mtu ambaye dhambi yake imeondolewa kabisa.
2 Heri mtu ambaye Mwenyezi-Mungu hamwekei hatia,mtu ambaye hana hila moyoni mwake.
3 Wakati nilipokuwa sijakiri dhambi yangu,nilikuwa nimedhoofika kwa kulia mchana kutwa.
4 Mchana na usiku mkono wako ulinilemea;nikafyonzwa nguvu zangu,kama maji wakati wa kiangazi.