4 Mchana na usiku mkono wako ulinilemea;nikafyonzwa nguvu zangu,kama maji wakati wa kiangazi.
5 Kisha nilikiri makosa yangu kwako;wala sikuuficha uovu wangu.Nilisema ninakuungamia makosa yangu ee Mwenyezi-Mungu,ndipo nawe ukanisamehe dhambi zangu zote.
6 Kwa hiyo, kila mwaminifu na akuletee maombi;jeshi likaribiapo au mafuriko,hayo hayatamfikia yeye.
7 Wewe ndiwe kinga yangu;wewe wanilinda katika taabu.Umenijalia shangwe za kukombolewa.
8 Mungu asema: “Nitakufunzana kukuonesha njia unayopaswa kufuata.Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.
9 Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,la sivyo hawatakukaribia.”
10 Watu waovu watapata mateso mengi,bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.