10 Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11 Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12 Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?
13 Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.
14 Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.
15 Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;
16 lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.