13 Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.
14 Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.
15 Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;
16 lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.
17 Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18 Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
19 Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.