16 lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.
17 Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18 Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
19 Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.
20 Huvilinda viungo vya mwili wake wote,hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.
21 Ubaya huwaletea waovu kifo;wanaowachukia waadilifu wataadhibiwa.
22 Mwenyezi-Mungu huokoa maisha ya watumishi wake,wote wanaomkimbilia hawataadhibiwa.