6 Maskini alimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamsikia,na kumwokoa katika taabu zake zote.
7 Malaika wa Mwenyezi-Mungu huwalinda wote wamchao,na kuwaokoa katika hatari.
8 Jaribuni mwone Mwenyezi-Mungu alivyo mwema.Heri mtu anayekimbilia usalama kwake.
9 Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.
10 Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11 Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12 Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?