1 Usihangaike kwa sababu ya waovu;usiwaonee wivu watendao mabaya.
2 Maana hao watatoweka mara kama nyasi;watanyauka kama mimea mibichi.
3 Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kutenda mema,upate kuishi katika nchi na kuwa salama.
4 Uitafute furaha yako kwa Mwenyezi-Mungu,naye atakujalia unayotamani moyoni.