25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee;kamwe sijaona mwadilifu ameachwa na Mungu,au watoto wake wakiombaomba chakula.
26 Daima huwapa wengine kwa furaha na kukopesha,na watoto wake ni baraka.
27 Achana na uovu, utende mema,nawe utaishi nchini daima;
28 maana Mwenyezi-Mungu hupenda uadilifu,wala hawaachi waaminifu wake.Huwalinda hao milele;lakini wazawa wa waovu wataangamizwa.
29 Waadilifu wataimiliki nchi,na wataishi humo milele.
30 Mtu mwadilifu husema maneno ya hekima,kwa ulimi wake hunena yaliyo ya haki.
31 Huizingatia moyoni mwake sheria ya Mungu wake;naye hatetereki katika mwenendo wake.