31 Huizingatia moyoni mwake sheria ya Mungu wake;naye hatetereki katika mwenendo wake.
32 Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;
33 lakini Mwenyezi-Mungu hatamtia mtu mwema makuchani mwake,wala kumwacha apatilizwe akishtakiwa.
34 Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kushika njia yake,naye atakukuza uimiliki nchi,na kuwaona waovu wakiangamizwa.
35 Nilimwona mwovu mdhalimu sana,alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!
36 Baadaye nikapita hapo, naye hakuwapo tena;nikamtafuta, lakini hakuonekana tena.
37 Mwangalie mtu mwema, mtu mwadilifu;mtu anayependa amani hujaliwa wazawa.