36 Baadaye nikapita hapo, naye hakuwapo tena;nikamtafuta, lakini hakuonekana tena.
37 Mwangalie mtu mwema, mtu mwadilifu;mtu anayependa amani hujaliwa wazawa.
38 Lakini wakosefu wote wataangamizwa;na wazawa wao watafutiliwa mbali.
39 Mwenyezi-Mungu huwaokoa waadilifu,na kuwalinda wakati wa taabu.
40 Mwenyezi-Mungu huwasaidia na kuwaokoa;huwatoa makuchani mwa waovu na kuwaokoa,maana wanakimbilia usalama kwake.