19 Maadui zangu hawajambo, wana nguvu;ni wengi mno hao wanaonichukia bure.
20 Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu,wananipinga kwa sababu natenda mema.
21 Usinitupe, ee Mwenyezi-Mungu;ee Mungu wangu, usikae mbali nami.
22 Uje haraka kunisaidia;ewe Mwenyezi-Mungu, uliye wokovu wangu.