8 Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.
9 Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.
10 Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.
11 Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.
12 Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.
13 Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.
14 Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.