1 Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu,nisije nikatenda dhambi kwa usemi wangu.Nitafunga mdomo wangu waovu wawapo karibu nami.”
2 Nilikuwa kama bubu, bila kusema kitu,nilinyamaza lakini sikupata nafuu.Mateso yangu yalizidi kuwa makali,
3 mahangaiko yangu yakaniunguza moyoni.Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika,kisha maneno haya yakanitoka:
4 “Ee Mwenyezi-Mungu, unijulishe mwisho wangu,siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi,nijue yapitavyo kasi maisha yangu!”