1 Nitakushukuru Mungu kwa moyo wangu wote;nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
2 Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mkuu.
3 Wakati ulipotokea, maadui zangu walirudi nyuma,walijikwaa na kuangamia.
4 Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.
5 Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.
6 Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.