4 Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;kiti cha enzi cha Mwenyezi-Mungu kiko mbinguni.Kwa macho yake huwachungulia wanadamu,na kujua kila kitu wanachofanya.
5 Mwenyezi-Mungu huwapima waadilifu na waovu;huwachukia kabisa watu wakatili.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberiti;upepo wa hari utakuwa ndio adhabu yao.
7 Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu na apenda uadilifu;watu wanyofu watakaa pamoja naye.