1 Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali?Kwani kujificha nyakati za shida?
2 Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali;Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza.
3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake,Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.
4 Mdhalimu kwa kiburi cha uso wakeAsema, Hatapatiliza.Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu;
5 Njia zake ni thabiti kila wakati.Hukumu zako ziko juu asizione,Adui zake wote awafyonya.
6 Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa,Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.
7 Kinywa chake kimejaa laana,Na hila na dhuluma.Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,