1 Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Mshukuruni Mungu wa miungu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17 Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 Akawaua wafalme mashuhuri;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 Sihoni, mfalme wa Waamori;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 Akaitoa nchi yao iwe urithi;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22 Urithi wa Israeli mtumishi wake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24 Akatuokoa na watesi wetu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25 Kila chenye mwili akipa chakula chake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.