27 Akaweka mambo ya ishara zake kati yao,Na miujiza katika nchi ya Hamu.
28 Alituma giza, kukafunga giza,Wala hawakuyaasi maneno yake.
29 Aliyageuza maji yao yakawa damu,Akawafisha samaki wao.
30 Nchi yao ilijaa vyura,Vyumbani mwa wafalme wao.
31 Alisema, kukaja makundi ya mainzi,Na chawa mipakani mwao mwote.
32 Badala ya mvua aliwapa mvua ya mawe,Na moto wa miali katika nchi yao.
33 Akaipiga mizabibu yao na mitini yao,Akaivunja miti ya mipaka yao.