30 Nchi yao ilijaa vyura,Vyumbani mwa wafalme wao.
31 Alisema, kukaja makundi ya mainzi,Na chawa mipakani mwao mwote.
32 Badala ya mvua aliwapa mvua ya mawe,Na moto wa miali katika nchi yao.
33 Akaipiga mizabibu yao na mitini yao,Akaivunja miti ya mipaka yao.
34 Alisema, kukaja nzige,Na tunutu wasiohesabika;
35 Wakaila miche yote ya nchi yao,Wakayala matunda ya ardhi yao.
36 Akawapiga wazaliwa wa kwanza katika nchi,Malimbuko ya nguvu zao.