6 Enyi wazao wa Ibrahimu, mtumishi wake;Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7 Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.
8 Analikumbuka agano lake milele;Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
9 Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka.
10 Alilomthibitishia Yakobo liwe amri,Na Israeli liwe agano la milele.
11 Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa.
12 Walipokuwa watu wawezao kuhesabiwa,Naam, watu wachache na wageni ndani yake,