20 Hulituma neno lake, huwaponya,Huwatoa katika maangamizo yao.
21 Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.
22 Na wamtolee dhabihu za kushukuru,Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.
23 Washukao baharini katika merikebu,Wafanyao kazi yao katika maji mengi,
24 Hao huziona kazi za BWANA,Na maajabu yake vilindini.
25 Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba,Ukayainua juu mawimbi yake.
26 Wapanda mbinguni, watelemka vilindini,Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya.