25 Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba,Ukayainua juu mawimbi yake.
26 Wapanda mbinguni, watelemka vilindini,Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya.
27 Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi,Akili zao zote zawapotea.
28 Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.
29 Huituliza dhoruba, ikawa shwari,Mawimbi yake yakanyamaza.
30 Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametuliaNaye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani.
31 Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.