29 Huituliza dhoruba, ikawa shwari,Mawimbi yake yakanyamaza.
30 Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametuliaNaye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani.
31 Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.
32 Na wamtukuze katika kusanyiko la watu,Na wamhimidi katika baraza ya wazee.
33 Amegeuza mito ikawa jangwa,Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu.
34 Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi,Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa.
35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji,Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.