3 Akawakusanya kutoka nchi zote,Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.
4 Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika;Hawakuona mji wa kukaa.
5 Waliona njaa, waliona na kiu,Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
6 Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.
7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka,Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.
8 Na wamshukuru BWANA, kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.
9 Maana hushibisha nafsi yenye shauku,Na nafsi yenye njaa huijaza mema.