32 Na wamtukuze katika kusanyiko la watu,Na wamhimidi katika baraza ya wazee.
33 Amegeuza mito ikawa jangwa,Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu.
34 Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi,Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa.
35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji,Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
36 Maana amewakalisha huko wenye njaa,Nao wametengeneza mji wa kukaa.
37 Wakapanda mbegu katika mashamba,Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake.
38 Naye huwabariki wakaongezeka sana,Wala hayapunguzi makundi yao.