35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji,Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
36 Maana amewakalisha huko wenye njaa,Nao wametengeneza mji wa kukaa.
37 Wakapanda mbegu katika mashamba,Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake.
38 Naye huwabariki wakaongezeka sana,Wala hayapunguzi makundi yao.
39 Kisha wakapungua na kudhilika,Kwa kuonewa na mabaya na huzuni.
40 Akawamwagia wakuu dharau,Na kuwazungusha katika nyika isiyo na njia.
41 Akamweka mhitaji juu mbali na mateso,Akamfanyia jamaa kama kundi la kondoo.