1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti,Nitaimba, nitaimba zaburi,Naam, kwa utukufu wangu.
2 Amka, kinanda na kinubi,Nitaamka alfajiri.
3 Ee BWANA, nitakushukuru kati ya watu,Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
4 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,Na uaminifu wako hata mawinguni.