12 Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili,Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake.
13 Wazao wake waangamizwe,Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.
14 Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za BWANA,Na dhambi ya mamaye isifutwe.
15 Ziwe mbele za BWANA daima,Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
16 Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili,Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,Hata akamfisha mtu aliyevunjika moyo,
17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata.Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye,
18 Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake.Ikamwingilia moyoni kama maji,Na kama mafuta mifupani mwake.