8 Siku zake na ziwe chache,Usimamizi wake na atwae mtu mwingine.
9 Wanawe na wawe yatima,Na mkewe na awe mjane.
10 Kutanga na watange wanawe na kuomba,Watafute chakula mbali na mahame yao.
11 Mdai na anase vitu vyote alivyo navyo,Wageni na wateke mapato ya kazi yake.
12 Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili,Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake.
13 Wazao wake waangamizwe,Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.
14 Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za BWANA,Na dhambi ya mamaye isifutwe.