5 Amewapa wamchao chakula;Atalikumbuka agano lake milele.
6 Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,Kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,Maagizo yake yote ni amini,
8 Yamethibitika milele na milele,Yamefanywa katika kweli na adili.
9 Amewapelekea watu wake ukombozi,Ameamuru agano lake liwe la milele,Jina lake ni takatifu la kuogopwa.