1 Haleluya.Heri mtu yule amchaye BWANA,Apendezwaye sana na maagizo yake.
2 Wazao wake watakuwa hodari duniani;Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.
3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali,Na haki yake yakaa milele.
4 Nuru huwazukia wenye adili gizani;Ana fadhili na huruma na haki.