4 Nuru huwazukia wenye adili gizani;Ana fadhili na huruma na haki.
5 Heri atendaye fadhili na kukopesha;Atengenezaye mambo yake kwa haki.
6 Kwa maana hataondoshwa kamwe;Mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Hataogopa habari mbaya;Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.
8 Moyo wake umethibitika hataogopa,Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9 Amekirimu, na kuwapa maskini,Haki yake yakaa milele,Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.