6 Kwa maana hataondoshwa kamwe;Mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Hataogopa habari mbaya;Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.
8 Moyo wake umethibitika hataogopa,Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9 Amekirimu, na kuwapa maskini,Haki yake yakaa milele,Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.