11 Enyi mmchao BWANA, mtumainini BWANA;Yeye ni msaada wao na ngao yao.
12 BWANA ametukumbuka,Naye atatubariki sisi.Ataubariki mlango wa Israeli,Ataubariki mlango wa Haruni,
13 Atawabariki wamchao BWANA,Wadogo kwa wakubwa.
14 BWANA na awaongeze ninyi,Ninyi na watoto wenu.
15 Na mbarikiwe ninyi na BWANA,Aliyezifanya mbingu na nchi.
16 Mbingu ni mbingu za BWANA,Bali nchi amewapa wanadamu.
17 Sio wafu wamsifuo BWANA,Wala wo wote washukao kwenye kimya;