2 Kwa nini mataifa kusema,Yuko wapi Mungu wao?
3 Lakini Mungu wetu yuko mbinguni,Alitakalo lote amelitenda.
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,Kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Zina vinywa lakini hazisemi,Zina macho lakini hazioni,
6 Zina masikio lakini hazisikii,Zina pua lakini hazisikii harufu,
7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi,Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 Wazifanyao watafanana nazo,Kila mmoja anayezitumainia.