7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi,Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 Wazifanyao watafanana nazo,Kila mmoja anayezitumainia.
9 Enyi Israeli, mtumainini BWANA;Yeye ni msaada wao na ngao yao.
10 Enyi mlango wa Haruni, mtumainini BWANA;Yeye ni msaada wao na ngao yao.
11 Enyi mmchao BWANA, mtumainini BWANA;Yeye ni msaada wao na ngao yao.
12 BWANA ametukumbuka,Naye atatubariki sisi.Ataubariki mlango wa Israeli,Ataubariki mlango wa Haruni,
13 Atawabariki wamchao BWANA,Wadogo kwa wakubwa.