3 Kamba za mauti zilinizunguka,Shida za kuzimu zilinipata.Naliona taabu na huzuni;
4 Nikaliitia jina la BWANA.Ee BWANA, nakuomba sana,Uniokoe nafsi yangu.
5 BWANA ni mwenye neema na haki,Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema.
6 BWANA huwalinda wasio na hila;Nalidhilika, akaniokoa.
7 Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako,Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.
8 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti,Macho yangu na machozi,Na miguu yangu na kuanguka.
9 Nitaenenda mbele za BWANAKatika nchi za walio hai.