10 Mataifa yote walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.
11 Walinizunguka, naam, walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.
12 Walinizunguka kama nyuki,Walizimika kama moto wa miibani;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.
13 Ulinisukuma sana ili nianguke;Lakini BWANA akanisaidia.
14 BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu,Naye amekuwa wokovu wangu.
15 Sauti ya furaha na wokovuImo hemani mwao wenye haki;Mkono wa kuume wa BWANA hutenda makuu.
16 Mkono wa kuume wa BWANA umetukuzwa;Mkono wa kuume wa BWANA hutenda makuu.