2 Israeli na aseme sasa,Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
3 Mlango wa Haruni na waseme sasa,Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
4 Wamchao BWANA na waseme sasa,Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
5 Katika shida yangu nalimwita BWANA;BWANA akanijibu akaniweka panapo nafasi.
6 BWANA yuko upande wangu, sitaogopa;Mwanadamu atanitenda nini?
7 BWANA yuko upande wangu, msaidizi wangu,Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
8 Ni heri kumkimbilia BWANAKuliko kuwatumainia wanadamu.