11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako,Nisije nikakutenda dhambi.
12 Ee BWANA, umehimidiwa,Unifundishe amri zako.
13 Kwa midomo yangu nimezisimuliaHukumu zote za kinywa chako.
14 Nimeifurahia njia ya shuhuda zakoKana kwamba ni mali mengi.
15 Nitayatafakari mausia yako,Nami nitaziangalia njia zako.
16 Nitajifurahisha sana kwa amri zako,Sitalisahau neno lako.
17 Umtendee mtumishi wako ukarimu,Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.