137 Ee BWANA, Wewe ndiwe mwenye haki,Na hukumu zako ni za adili.
138 Umeziagiza shuhuda zako kwa haki,Na kwa uaminifu mwingi.
139 Juhudi yangu imeniangamiza,Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako.
140 Neno lako limesafika sana,Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.
141 Mimi ni mdogo, nadharauliwa,Lakini siyasahau mausia yako.
142 Haki yako ni haki ya milele,Na sheria yako ni kweli.
143 Taabu na dhiki zimenipata,Maagizo yako ni furaha yangu.