144 Haki ya shuhuda zako ni ya milele,Unifahamishe, nami nitaishi.
145 Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee BWANA, uitike;Nitazishika amri zako.
146 Nimekuita Wewe, uniokoe,Nami nitazishika shuhuda zako.
147 Kutangulia mapambazuko naliomba msaada,Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148 Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku,Ili kuitafakari ahadi yako.
149 Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako,Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150 Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.