146 Nimekuita Wewe, uniokoe,Nami nitazishika shuhuda zako.
147 Kutangulia mapambazuko naliomba msaada,Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148 Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku,Ili kuitafakari ahadi yako.
149 Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako,Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150 Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.
151 Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.
152 Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako,Ya kuwa umeziweka zikae milele.