151 Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.
152 Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako,Ya kuwa umeziweka zikae milele.
153 Uyaangalie mateso yangu, uniokoe,Maana sikuisahau sheria yako.
154 Unitetee na kunikomboa,Unihuishe sawasawa na ahadi yako.
155 Wokovu u mbali na wasio haki,Kwa maana hawajifunzi amri zako.
156 Ee BWANA, rehema zako ni nyingi,Unihuishe sawasawa na hukumu zako.
157 Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi,Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.